MBUZI WA ZAWADI YA WAZIRI MKUU AIBIWA KABLA YA KUKABIDHIWA IRAMBA
Na Arusha Digital | Singida
Katika tukio la kushangaza lililozua mjadala miongoni mwa wananchi na viongozi, mbuzi aliyekuwa ameandaliwa kama zawadi maalum kwa Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, kutoka kwa wananchi wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, ameibwa muda mfupi kabla ya kukabidhiwa rasmi.
Tukio hilo limetokea leo, Juni 13, 2026, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wilayani humo, ambapo wananchi walikuwa wameandaa mbuzi huyo kama ishara ya shukrani, heshima na kuthamini mchango wa Serikali katika maendeleo ya eneo hilo.
Kwa mujibu wa taarifa za awali, mbuzi huyo alitoweka katika mazingira ambayo bado hayajafahamika, muda mfupi kabla ya ratiba ya kukabidhi zawadi hiyo kutekelezwa mbele ya viongozi na wananchi waliojitokeza kwenye hafla hiyo.
Wakizungumza baada ya tukio hilo, baadhi ya wananchi walieleza kusikitishwa na kilichotokea, wakisema kiliharibu maandalizi yaliyokuwa yamefanywa kwa lengo la kumuenzi na kumpongeza Waziri Mkuu wakati wa ziara yake.
Tukio hilo pia limewaacha viongozi wa eneo hilo katika mshangao, huku vyombo husika vikianza kufuatilia mazingira ya kutoweka kwa mbuzi huyo ili kubaini waliohusika na hatua stahiki zichukuliwe.
Hadi kufikia muda wa kuandikwa kwa habari hii, mbuzi huyo alikuwa hajapatikana, huku uchunguzi ukiendelea kubaini ukweli wa tukio hilo ambalo limeibua hisia na maswali mengi miongoni mwa wakazi wa Iramba.
Ends..


إرسال تعليق