Na Joseph Ngilisho – Arumeru
VIONGOZI wa mila, dini na wanasiasa wilayani Arumeru wamefanya maombi maalumu ya kulaani vurugu na umwagaji damu uliotokea katika maandamano kufuatia uchaguzi wa Oktoba 29, huku wakitoa onyo kali kwa wananchi—hasa vijana—kujiepusha na maandamano hayo wanayoyaita “chanzo cha machafuko na kurudisha nyuma maendeleo.”
Mkutano huo ulifanyika leo Dc 6,2025 katika Mti maarufu wa jadi wa Mringaringa, uliopo Kata ya Poli, ambapo Mshiri Mkuu wa jadi ya Wameru, Willson Mbise, alitoa tamko zito akisisitiza kuwa jamii ya Wameru haitasita kuwachukulia hatua wale wote watakaohamasisha au kushiriki maandamano.
> “Atakayethubutu kurudia kitendo cha maandamano tutamchukulia hatua,” alisema kwa msisitizo.
>
“Sasa nyinyi Wameru mnadanganywa ili mjikaange wenyewe. Mimi nawaomba kama kiongozi wenu msikubali. Vita haina maendeleo,” alisema Mbise.
Akizungumza katika Mkutano huo, Nasari aliwashukuru wananchi kwa kumuamini na kumchagua, akiahidi kuongoza kwa misingi ya maendeleo na uwajibikaji wa kweli.
>
“Mimi ni mbunge wa maendeleo. Sitaki kuwa mbunge wa kutatua shida za mtu mmoja mmoja,” alisema.
Alionya tabia ya baadhi ya watu kumualika katika makundi ya michango ya harusi, kwaya na sherehe mbalimbali, akisisitiza kwamba jukumu lake kubwa ni kuleta maendeleo ya pamoja na kushughulikia kero za wananchi wa Meru.
Akirejea tukio la vurugu lililotokea majuzi, Nasari alisema limekumbusha wajibu mkubwa ulio mbele yao kama viongozi.
> “Awamu hii, kwa sisi mliotuchagua, tutawafanya muone maendeleo ambayo hamjawahi kuyaona,” aliahidi.
>
“Uongozi wetu huu, na mimi nikiwa nimepewa fimbo ya kuwaongoza, nitahakikisha tunawajibika kweli kweli—usiku na mchana—kuwatumikia wananchi,” alisema.
Ends...




















0 Comments