By Arushadigital
Rais wa Marekani Donald Trump amesema Marekani imefanya “mashambulizi makubwa” dhidi ya Venezuela na kwamba imemkamata Rais wa nchi hiyo, Nicolás Maduro, pamoja na mke wake.
Katika taarifa aliyochapisha kwenye mtandao wa Truth Social, Trump alisema: “Marekani imefanikiwa kutekeleza mashambulizi makubwa dhidi ya Venezuela na kiongozi wake, Rais Nicolás Maduro, ambaye yeye pamoja na mke wake wamekamatwa na kusafirishwa nje ya nchi.”
Trump aliongeza kuwa operesheni hiyo ilifanyika kwa kushirikiana na vyombo vya usalama vya Marekani, akisema maelezo zaidi yatatolewa baadaye. Pia ametangaza kutakuwa na mkutano na waandishi wa habari lbaadaye katika makazi yake ya Mar-a-Lago.
Hadi sasa, serikali ya Venezuela haijatoa tamko rasmi kuthibitisha au kukanusha madai hayo ya kukamatwa kwa maduro.
Maafisa wameiambia CBS News, mshirika wa BBC nchini Marekani, kwamba Maduro, amekamatwa na kikosi cha Delta Force cha jeshi la Marekani. Delta Force ni kikosi cha juu kabisa cha jeshi la Marekani kinachojihusisha na operesheni za kupambana na ugaidi.
Ends..


0 Comments