MAAFISA WA ULINZI KUTOKA NCHI 17 WAHUDHURIA MAFUNZO YA KIMATAIFA YA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI NDC ARUSHA

 Na Joseph Ngilisho, Arusha


BALOZI Meja Jenerali Wilbert Ibuge, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC), amesema ziara ya maafisa waandamizi kutoka nchi 17 barani Afrika na nje ya bara inayoendelea jijini Arusha inalenga kujifunza kwa vitendo namna sekta ya utalii na uchumi zinavyounganishwa na masuala ya usalama wa taifa.

Akizungumza leo Novemba 10,2025  baada ya  kupokea ugeni huo mzito wa maafisa waandamizi wa vyombo vya ulinzi na usalama kutoka nchi 17 za Afrika na nje ya Afrika , mkuu wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla, amewahakikishia usalama na utulivu siku zote tano wawapo mkoani hapa,katika  kushiriki mafunzo ya Chuo cha Taifa cha Ulinzi (National Defence College – NDC).


RC Makalla alisisitiza kuwa Mkoa wa Arusha unaendelea kuwa ngome ya utulivu na amani inayochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

>

“Arusha ni kitovu cha utalii na uchumi wa Kanda ya Kaskazini. Nawakaribisha mjisikie mko nyumbani. Mkoani kwetu kuna usalama wa kutosha kutokana na ushirikiano mzuri uliopo kati ya wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama,” alisema CPA Makalla.


Ujumbe huo wa maafisa wa NDC unaongozwa na Balozi Meja Jenerali Wilbert Ibuge, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi, ambaye aliambatana na wakufunzi wandamizi elekezi pamoja na washiriki wa kozi ndefu ya 14 ya chuo hicho iliyoanza Septemba hadi Julai 2026 .

Mataifa yanayoshiriki mafunzo hayo ni pamoja na mwenyeji Tanzania, kenya, Uganda, malawi, Namibia, Zambia, Botswana, zimbabwe, Bangladesh, south Africa, India, Egypt, Sierra Leone, Ethiopia,Burundi, Rwanda pamoja na Nigeria.

Alisema kuwa lengo la ziara hiyo jijini Arusha ni kujifunza kwa vitendo namna sekta ya utalii na uchumi zinavyounganishwa na masuala ya usalama wa taifa kwa sababu wanafunzi wanafanya mafunzo katika usalama wa taifa na mikakati.

"Ni kawaida kila mwaka chuo chetu kutembea Arusha hususani ndio kitovu cha taifa kwenye sekta ya utalii lengo ni kuelewa kitovu cha utalii kinaendeleaje na mikakati yake"


Katika programu hiyo inayojulikana kama “Tentative Programme for Economy in Tourism”, washiriki wanatarajiwa kutembelea taasisi na vivutio muhimu vya utalii ikiwemo Makao Makuu ya TANAPA, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) pamoja na maeneo ya kihistoria na kitamaduni ndani ya Jiji la Arusha.


Kwa mujibu wa Mkuu wa NDC, Meja Jenerali Ibuge, mafunzo hayo yanawapa washiriki fursa ya kujifunza uhusiano kati ya utalii, uchumi na usalama wa kikanda, sambamba na kubadilishana uzoefu wa kitaaluma miongoni mwa nchi wanachama.

>

“Tunataka washiriki wetu waone namna Tanzania inavyotumia rasilimali zake za utalii kwa manufaa ya kiuchumi bila kuhatarisha usalama wa taifa. Arusha ni mfano bora wa uhusiano huo,” alisema Meja Jenerali Ibuge.


Mafunzo hayo ya NDC ni sehemu ya mfululizo wa programu za kimkakati zinazolenga kukuza ushirikiano wa kikanda katika masuala ya ulinzi, usalama na maendeleo endelevu.











 




-ends..





Post a Comment

0 Comments