THE PICNIC BAR YAJITENGA NA TUKIO LA KIFO CHA ASKARI POLISI,TAARIFA SAHIHI NI KWAMBA ALIUAWA KATIKA ENEO LA BAR YA SIMALOI NA SIO PICNIC KAMA ILIVYORIPOTIWA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII SAMAHANI KWA USUMBUFU!

 

TAARIFA KWA UMMA

BAA YA PICNIC HAIHUSIKI NA TUKIO LA KIFO CHA ASKARI POLISI  KAMA ILIVYORIPOTIWA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII

Na Arushadigital — Arusha

 

Uongozi wa Picnic Bar iliyopo eneo la Kaloleni jijini Arusha umetolea ufafanuzi taarifa zilizokuwa zikisambaa mitandaoni zikidai kuwa tukio la kuuawa kwa askari polisi aliyetajwa kwa jina la Omari Mnandi lilitokea katika eneo la baa hiyo.

Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, uongozi wa Picnic Bar umekanusha vikali taarifa hizo na kubainisha kuwa tukio hilo halikutokea katika eneo la baa hiyo, bali lilitokea katika bar ya Simaloi ambayo pia ipo eneo la Kaloleni jijini Arusha.

> “Tunapenda kueka wazi kwa wateja wetu na umma kwa ujumla kwamba tukio hilo la kusikitisha halikutokea katika baa yetu. Picnic Bar haikuhusishwa kwa namna yoyote na tukio hilo. Samahani kwa usumbufu na taharuki iliyosababishwa na taarifa hizo zisizo sahihi,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Askari Omari Mnandi aliyeuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani

Uongozi wa baa hiyo pia umewataka wananchi na wadau wa vyombo vya habari kuwa makini katika utoaji na usambazaji wa taarifa, ili kuepuka kuharibu taswira ya taasisi au biashara zinazohusishwa kimakosa na matukio.

> “Tunaendelea kutoa huduma zetu kama kawaida katika mazingira tulivu na salama, na tunawakaribisha wateja wote bila wasiwasi,” imeongeza taarifa hiyo.


Awali, mitandao kadhaa ya kijamii na vyombo vya habari viliripoti kimakosa kwamba askari huyo alipigwa na kitu kizito kichwani katika baa ya Picnic, jambo ambalo sasa limebainika kuwa si kweli.

Arushadigital ni chombo kinachofanya kazi kwa weledi na kuzingatia maadili  hivyo basi tunawasihi wasomaji wetu muendelee kutufuatilia kwa habari za ukweli na uhakika

Uchunguzi wa vyombo vya usalama umeonyesha kwamba tukio hilo lilitokea katika baa ya Simaloi, eneo hilo hilo la Kaloleni, jijini Arusha.

Mwisho.

-ends

Post a Comment

0 Comments