CCM Yazindua Kampeni kwa Kishindo Arumeru Magharibi
Na Joseph Ngilisho, ARUMERU
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) jimbo la Arumeru Magharibi limezindua kampeni zake kwa kishindo, likimnadi mgombea wake wa ubunge, Dkt. Johannes Lukumay, pamoja na wagombea udiwani wa kata zote 27 za jimbo hilo.
Uzinduzi huo uliofanyika katika viwanja vya Ngaramtoni ulihudhuriwa na maelfu ya wananchi na wafuasi wa chama hicho, huku shamrashamra, nyimbo za wasanii na nderemo zikisindikiza tukio hilo. Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Stephen Wasira, ndiye aliyekuwa mgeni rasmi.
Wasira: Serikali ya Samia imetekeleza miradi mikubwa
Aidha, alibainisha kuwa mchakato wa kumpata mgombea ubunge kupitia kura za maoni ndani ya CCM ni mfumo wa haki na wa kidemokrasia ambao umeendelea kuwa mfano wa kuigwa, tofauti na vyama vingine vya siasa.
Lukumay: Tuungane kupiga vita umasikini
> “Kinachotakiwa sasa ni mshikamano na bidii ya kazi. Lazima tuungane kuuchukia umasikini na kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi wa jimbo hili,” alisema.
CCM yahimiza mshikamano
Uzinduzi huo umeashiria kuanza kwa mbio kali za kisiasa Arumeru Magharibi, huku CCM ikijipanga kuhakikisha inabaki kuwa chaguo la wananchi.
Ends…
0 Comments