BODI YANG'AKA, YAMREJESHA MADARAKANI KATIBU MKUU TWARIQA, SHEIKH HARUNA HUSEIN ,YATOA ONYO KALI KWA MWENYEKITI
Na Joseph Ngilisho | ARUA
Bodi hiyo imesema mamlaka ya kuchukua hatua dhidi ya viongozi wa taasisi hiyo yanapaswa kutekelezwa na chombo chenye dhamana kwa mujibu wa Katiba , kanuni na taratibu zilizowekwa , na kwamba hakuna kiongozi mmoja anayepaswa kujichukulia mamlaka ya kufanya maamuzi makubwa bila kuwashirikisha wahusika wenye mamlaka.
Akizungumza mapema leo Sep 5,2026 kuhusu uamuzi huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini, Shaffi Ali Mkande, amesema baada ya kulijadili suala la kuondolewa kwa Sheikh Haruna kwa kina, Bodi ilibaini kuwepo kwa ukiukwaji wa utaratibu na hivyo kuamua kumrejesha rasmi katika nafasi yake.“Bodi imejadili suala hili na kuona kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa utaratibu katika kumuondoa Katibu Mkuu. Kwa hiyo, tunatangaza kwamba Sheikh Haruna Husein anaendelea na nafasi yake ya Katibu Mkuu wa Taifa,” amesema Mkande.
Bodi pia imemtaka Sheikh Salimu Mubaraka kuacha kujichukulia mamlaka na kusisitiza kuwa uongozi wa taasisi hauwezi kuendeshwa kwa maamuzi ya mtu mmoja bila kushirikisha vyombo vilivyopewa dhamana.
ULAMAA WAKATAA KUSIMAMISHWA KWA KATIBU
Muhonzi amesema maamuzi yanayohusu taasisi yanapaswa kufanywa baada ya viongozi husika kukaa pamoja, kushauriana na kufikia uamuzi kwa kuzingatia Katiba na misingi ya Qur’ani.
“Katika dini, tunapotaka kufanya jambo lazima tushauriane. Mashauriano kwanza, kisha ndiyo tufanye lile jambo,” amesema.
Amesema kutokuwepo kwa mashauriano ndiko kulikosababisha mvutano uliopo, akisisitiza kuwa hata Katiba ya taasisi iliyotungwa na binadamu inapaswa kutekelezwa kwa kuzingatia misingi ya Qur’ani.
Amesema mamlaka ya kushughulikia masuala ya viongozi yako chini ya vyombo vilivyowekwa na taasisi, hivyo matamko yanayotolewa bila kufuata utaratibu hayawezi kuwa na uhalali wa kiuongozi.
“Sisi kama Bodi ya Wadhamini hatutambui tamko lile. Waliotangaza hawakuwa na mamlaka ya kufanya hivyo, kwa sababu mwenye mamlaka ya kutoa tamko kama hilo anajulikana,” amesema Athuman.
Athuman amewataka viongozi wa dini kutumia nafasi zao kuimarisha amani na utulivu, akisisitiza kuwa hawapaswi kutoa kauli au kuchukua hatua zinazoweza kuongeza taharuki katika jamii.
Amesema Bodi iko tayari kukemea vitendo vinavyoweza kuvuruga amani na mshikamano, huku ikisisitiza umuhimu wa viongozi wa dini kushirikiana katika kutatua tofauti kwa njia ya mazungumzo na mashauriano.
...Ends..










إرسال تعليق