TAMBO LA MGOMBEA UDIWANI OLASITI BAADA YA KUCHUKUA FOMU ,AFUNGA MITAA KWA MAANDAMANO,ATAMBA YEYE NI DIWANI WA KITAIFA AWATAKA WANAOLASITI KUTEMBEA VIFUA MBELE!


MGOMBEA UDIWANI OLASITI ATOA TAMBO ZA USHINDI BAADA YA KUTEULIWA RASMI

Na Joseph Ngilisho- ARUSHA 


HALI ya shamrashamra na nderemo ilitawala mapema  leo  katika Kata ya Olasiti, jijini Arusha, baada ya mgombea udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Alex Martin, kuchukua fomu ya uteuzi wake rasmi, akifuatana na umati mkubwa wa wanachama na wafuasi wa chama hicho.

Martin ambaye alikuwa akitetea kiti chake cha udiwani, awali alishindwa kwenye kura za maoni, lakini baadaye jina lake lilipendekezwa na Kamati Kuu ya CCM kutokana na vigezo mbalimbali ikiwemo uadilifu, utendaji wake na mchango mkubwa katika maendeleo ya kata hiyo.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu mapema le Agosti 19,2025, Martin aliwashukuru wanachama wa CCM na wananchi kwa kuendelea kumuunga mkono, akiahidi kuendeleza miradi ya maendeleo aliyoipeleka Olasiti katika kipindi cha uongozi wake wa awali.

Aidha Martin alisema Olasiti bado inamhitaji na alishukuru mchakato uliofanyika kuanzia Ngazi ya wilaya , Mkoa hadi Taifa ambao ndio wamerejesha jina lake baada ya mchakato mkali na hivyo alisisitiza kuwa yeye ni diwani wa kitaifa .Amewataka wananchi wa Olasiti Kutembea vifua mbele kwa kuwa mtetezi wao bado U hai.

>

“Najua tumepitia changamoto kwenye mchakato wa kura za maoni, lakini chama kimeona bado nina jukumu la kuwatumikia watu wa Olasiti .Nawaahidi sitawaangusha, bali nitaongeza kasi ya maendeleo, huduma bora na mshikamano wa wananchi,” alisema Martin huku akishangiliwa na umati wa wafuasi wake.


Wafuasi waliomsindikiza walibeba mabango yenye jumbe za kumpongeza na kuonyesha imani kwa uongozi wake. Baadhi walionekana wamevalia sare za kijani na njano huku wakipiga ngoma na kuimba nyimbo za hamasa.

Mwenyekiti wa ccm Kata ya Olasiti,Frank Sakachi aliwashukuru wanachama wa ccm kwa kujitokeza kwa wingi kumsindikiza mgombea huyo katika mchakato wa kuchukua fomu,Amewataka kuvunja makundi na kuendeleza mshikamano wa kumtafutia kura ili kuhakikisha mgombea huyo anashinda.








Ends ..

Post a Comment

0 Comments