Breaking🔥

DAKTARI BINGWA ALIYEMTWANGA MAKONDE TRAFIKI AFIKISHWA MAHAKAMANI

DAKTARI BINGWA  ALIYEMTWANGA MAKONDE TRAFIKI AFIKISHWA MAHAKAMANI 

Na Joseph Ngilisho | Dar es Salaam

     
DAKTARI bingwa wa magonjwa ya ndani katika Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Conrad Agonza Kahyoza, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni, jijini Dar es Salaam, kwa tuhuma za kumshambulia askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani akiwa katika utekelezaji wa majukumu yake.

Dkt. Kahyoza amefikishwa mahakamani leo, Septemba 10, 2026, baada ya kukamatwa na Jeshi la Polisi kufuatia tukio linalodaiwa kutokea katika Barabara ya Bagamoyo, eneo la Lugalo, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, tukio hilo lilitokea Jumanne, Septemba 8, 2026, majira ya saa 1:30 asubuhi.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa wakati wa tukio hilo, askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani mwenye namba F.8886 SGT Andrew, alikuwa akitekeleza majukumu yake ya kudhibiti magari yaliyokuwa yakitumia barabara ya huduma (Service Road) kinyume na utaratibu.

Katika mazingira hayo, Dkt. Kahyoza anadaiwa kuhusika katika tukio lililomlenga askari huyo, hali iliyosababisha Polisi kumkamata na baadaye kumfikisha mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.

Dkt. Kahyoza alionekana katika chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni huku taratibu za kisheria zikiendelea kuhusu tuhuma zinazomkabili.

Hata hivyo, tuhuma hizo bado ni madai ambayo hayajathibitishwa na mahakama. Dkt. Kahyoza anapaswa kuchukuliwa kuwa hana hatia hadi pale mahakama itakapothibitisha vinginevyo kwa mujibu wa sheria.

Ends..

Post a Comment

أحدث أقدم