Na Joseph Ngilisho-LONGIDO
NAIBU waziri Mkuu na waziri wa Nishati dkt Dotto Biteko amempongeza Mchimbaji wa madini ya Rubby Bilionea Sendeu Laizer kutoka kabila dogo la wamasai wilayani Longido akidai ni miongoni mwa wazawa wachache wanaofanya vizuri katika sekta hiyo hapa nchini, ambaye ameweza kuchangia zaidi ya sh, bilioni 3 kwa huduma za kijamii pamoja na kodi ya serikali.
Dkt Biteko ametoa pongezi hizo leo Aprili 22,2025 wakati akihutubia mamia ya wananchi wakiwemo wachimbaji wa madini ya Rubby katika kijiji cha Mundarara wilayani Longido mkoani Arusha na kueleza kuwa wachimbaji wazawa wakiwezeshwa kwa kujengewa mazingira mazuri wanaweza kulipeleka mahala pasuri zaidi Taifa letu.
Alisisitiza kuwa sekta ya madini ni kichocheo kikubwa katika maendeleo ya ukuaji wa kiuchumi na kuwa kijiji cha Mundarara kimekuwa na uzalishaji wa madini ambayo yanapaswa kuwanufaisha wazawa.
"Kuna watu fulani wamekuwa wakiaminisha kuwa Madini hayawezi kuchimbwa na Masai,anatakiwa kuja mtu fulani kutoka kwingine na ndiye anayeweza kuchimba na kukuza uchumi wa Madini "
"Leo hii nimesimama hapa nikiwa mwenye furaha sana kukutana na ndugu yangu Sendeu tangua ameanza kusoma hotuba yake anataja mamilioni na mabilioni anayochangia uchumi wa Taifa,hii inatupa heshima kama Taifa watanzania wakiwezeshwa na kupewa fursa ya kusimamia uchumi wao wanaweza"
"Ninarudi leo nikiwa na furaha uchumi unaosimamiwa na wana Mundarara niwakutiliwa mfano na kazi ya serikali ni kutatua haraka Changamoto za wachimbaji na Wafanyabiashara wa madini jambo la kutoa huduma kwa wananchi sio hisani ni Lazima"Alisema Biteko.
Katika hatua nyingine dkt Biteko aliagiza shirika la Umeme Tanzania(Tanesco) kuhakikisha wanapeleka na kufunga Transfoma kubwa katika kijiji cha Mundarara ili kuwasaidia wananchi na wachimbaji wa Madini hayo kuwa na umeme wa uhakika wenye uwezo mkubwa wa kuendesha mitambo ya uzalishaji mgodini tofauti na sasa umeme uliopo unauwezo mdogo.
Awali Mchimbaji wa madini ya Rubby Bilionea Sendeu Laizer akisoma taarifa yake kwa naibu waziri Mkuu Biteko, alimweleza waziri huyo namna wanavyopata Changamoto ya umeme na mahitaji yao ya Transfoma itakayowezesha kupatikana kwa umeme utakaokuwa na uwezo wa kuendesha mitambo yao ya migodini.
"Tunamwomba naibu waziri Mkuu Dkt Doto biteko atufanyie wepesi tuweze kupata Transifoma pamoja na zahanati ambayo ndio hitaji kubwa kwa sasa katika eneo hilo la Mundarara"
Sendeu kupitia kampuni yake ya Sendeu Agrovet Co. Ltd na mwekezaji mzawa ametoa madawati 300 yenye thamani ya sh,milioni 40 kwa ajili ya kusaidia shule tano za kata ya mundarara.
Alisema hatua hiyo ni kutokana na kurudisha faida kidogo kwa jamii kwani kupitia sekta hiyo wamenufaika nayo huku akiomba kituo cha afya katika kata hiyo kwa aajili ya wachimbaji madini na wananchi kupata huduma bora za afya .
Pia Laiser alisema kuwa amekuwa akichimba madini ya Rubbi na kuuza kwa kufuata sheria na ameweza kutumia kiasi cha sh,milioni 547 kusaidia shughuli za kijamii inayomzunguka na amelipa kodi ya Serikali kiasi cha zaidi ya sh,bilioni 2 .
Ends....
0 Comments