MBUNGE DR. LUKUMAY AKETI MEZA MOJA NA RAIS SAMIA, AJADILI MASUALA YA AFYA

 MBUNGE DR. LUKUMAY AKETI MEZA MOJA NA RAIS SAMIA, AJADILI MASUALA YA AFYA

Na Joseph Ngilisho-Arushadigital| Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameongoza viongozi na wataalamu mbalimbali wa afya kushiriki Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu, uliofanyika katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), jijini Dar es Salaam, Aprili 16, 2026.

Mkutano huo mkubwa wa kimataifa umewakutanisha wataalamu wa afya kutoka mataifa mbalimbali duniani, ukilenga kujadili maendeleo ya sayansi ya tiba, kubadilishana uzoefu pamoja na kuimarisha huduma za upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu.

Miongoni mwa viongozi wa kitaifa waliopata fursa ya kushiriki katika mkutano huo ni Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Dkt Johannes Lembulung Lukumay, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI. Dr. Lukumay alionekana akiwa katika meza moja na Rais Samia, hatua inayoashiria umuhimu wa ushirikiano kati ya mihimili ya dola katika kuimarisha sekta ya afya nchini.

.ends..

Post a Comment

0 Comments