By Arushadigit
Serikali ya Australia imetangaza uteuzi wa kihistoria wa mwanamke kuwa Mkuu wa Jeshi la Nchi hiyo kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwake. Uteuzi huu unakuja wakati Jeshi likikabiliwa na changamoto za unyanyasaji wa kijinsia na ubaguzi dhidi ya wanawake.
Luteni Jenerali Susan Coyle anatarajiwa kuanza rasmi kazi yake kama Mkuu wa Jeshi mnamo Julai 2026, akichukua nafasi ya Simon Stuart. Waziri Mkuu Anthony Albanese ameeleza kuwa hii ni hatua muhimu katika historia ya Jeshi la Australia lenye zaidi ya miaka 125, na kwamba uteuzi huu unaweza kufungua milango kwa wanawake wengi zaidi kujiunga na Jeshi.
Aidha, Waziri wa Ulinzi Richard Marles ametaja uteuzi huu kama hatua kubwa, akisema mafanikio ya Coyle yatahamasisha wanawake waliopo Jeshini pamoja na wale wanaotaka kujiunga siku za usoni. Hivi sasa wanawake wanachangia takriban asilimia 21 ya majeshi yote na asilimia 18.5 ya nafasi za juu za uongozi, huku Serikali ikiweka lengo la kufikia asilimia 25 ifikapo mwaka 2030.

0 Comments