By Arushadigital- Dar Es Salaam
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda, amempandisha cheo Alphonce Simbu kutoka Sajini kuwa Sajinitaji katika hafla iliyofanyika ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi Upanga Jijini Dar es Salaam leo Septemba 25, 2025 baada ya kupata mafanikio ya Mbio za Marathon Tokyo, Japan.
Jenerali Mkunda amesema ushindi wa Simbu wa kutwaa medali ya dhahabu katika Mashindano ya Mbio za Marathon ya Dunia Kilomita 42, zilizofanyika Toyo Japan ni kwa Watanzania wote na Afrika kwa ujumla na kwamba michezo ni sehemu ya kazi jeshini, hivyo Sajinitaji Alphonce Simbu amefanya kazi nzuri na kuwataka Maafisa na Askari wote jeshini kuiga mfano wa Sajinitaji Simbu.
Pamoja na pongezi hizo, Jenerali Mkunda amempandisha cheo kutoka Sajini kuwa Sajinitaji tukio lililofanyika ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi Upanga Jijini Dar es Salaam leo Septemba 25, 2025.
Jenerali Mkunda amesema ushindi huu ni kwa Watanzania wote na Afrika kwa ujumla na kwamba michezo ni sehemu ya kazi jeshini, hivyo Sajinitaji Alphonce Simbu amefanya kazi nzuri.
Jenerali Mkunda ametoa rai kwa maafisa na askari wote jeshini kuiga mfano wa Sajinitaji Simbu kwa kufanya kazi kwa bidii na kuleta mafanikio katika kila idara jeshini.
Ends..
0 Comments