TARURA KUTUMIA BILIONI 2 MATENGENEZO YA BARABARA KWA KIWANGO CHA LAMI JIJI LA ARUSHA

Na Joseph Ngilisho- ARUSHA 

Wakala wa Barabara za mijini na Vijini TARURA  inatarajia kutumia kiasi cha sh, bilioni mbili kukamilisha Ujenzi wa Barabara ya TCA Levolosi,CCM, Kaloleni-KwaBenson na TRA Hadi East Africa Zenye Urefu wa Kilomita 2.241 na zitakazojegwa kwa kiwango Cha Lami katikati ya jiji la Arusha.


Hayo yamesemwa wakati Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 ulipotembelea na kuweka jiwe la Msingi Katika Mradi huo.

Akisoma Taarifa ya Ujenzi huo Mbele ya Kiongozi Wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2025 Ismail Ali Ussi ,meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Wilaya ya Arusha Mhandisi Godfrey Bwire amesema Mradi huo ulianza kutekelezwa juni 28,2024 huku ukitarajia kukamilika Mwaka huu. 

Meneja huyo wa Tarura amesema Ujenzi huo wa Barabara unalenga  kusogeza Huduma  ya Miundombinu ya Barabara Kwenye Makazi ya Watu ili kurahisisha Huduma za Usafirishaji kwa kupunguza Gharama za Maisha. 


Akizungumza kabla ya kuweka Jiwe la Msingi Katika Barabara hiyo Kiongozi Wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  Kitaifa Ismail Ali Ussi  ameipongeza Tarura kwa kuendelea kumwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza Ahadi za kuboresha Miundombinu pamoja na Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi wa Barabara kuwa na Ubora unatakiwa.

Aidha Barabara zinazojengwa kwa kiwango Cha Lami ni TCA 0.655 km,Levolosi 0.187km,CCM 0.129km,Kaloleni Hadi Kwa Benson 1.0km na TRA Hadi East Afrika 0.27km.

Post a Comment

0 Comments