CHUO CHA UFUNDI ARUSHA ATC CHAZINDUA MAABARA YA TEKNOLOJIA YA UCHAPAJI YA 3D YENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 70.

Na Joseph Ngilisho-ARUSHA

CHUO  cha Ufundi Arusha (ATC) kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Korea (KOICA) , kimezindua rasmi  Maabara ya kisasa ya Kwanza ya aina yake hapa nchini yenye  Teknolojia ya uchapishaji wa 3D.


Maabara hiyo ni zao la mashirikiano baina ya chuo cha Arusha na Nchi ya Korea katika  kuimarisha mafunzo ya Uhandisi wa Kidigitali yatakayochochea ubunifu kwa wanafunzi .


Mkurugenzi wa KOICA nchini Tanzania, Manshik Shin, alisema kuwa maabara hiyo ni sehemu ya juhudi za shirika lake kusaidia maendeleo ya elimu ya ufundi nchini kwa kuzingatia mahitaji ya sasa ya soko la ajira.



Alisema maabara hiyo imelenga kufundisha na kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kutumia teknolojia mpya zinazotumika kwenye viwanda vya kisasa nchini na nje ya nchi.


"Maabara hii ya kisasa imejengwa kwa gharama ya Dola za Kimarekani 28,000 kwa ushirikiano kati ya ATC na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Korea (KOICA),"alisema.


Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha,  Musa Chacha, alisema kuwa uwepo wa maabara hiyo, ni hatua kubwa kwa chuo na taifa kwa ujumla, hasa katika kuandaa wahandisi na mafundi stadi watakaokuwa tayari kwa soko la ajira linalobadilika kwa kasi.



Uzinduzi huo ni sehemu ya mpango mpana wa kuimarisha elimu ya ufundi stadi nchini, kwa lengo la kuandaa vijana kwa ushindani katika soko la ajira la kimataifa na kuchochea ubunifu na ujasiriamali katika teknolojia.

Chacha aliongeza, "Hii ni rasilimali ya pamoja ambayo inawakilisha roho ya ushirikiano na maendeleo. Uwekezaji wa KOICA utasaidia sana katika kuendeleza mafunzo ya kiufundi, utafiti, na uvumbuzi."


Akiwakilisha baraza la wanafunzi, Elisha  Mwakitaja kutoka Idara ya Mechatronics and Materials Engineering (NTA Level 8) alitoa ya moyoni kwa niaba ya wenzake:

"Kama mwakilishi wa wanafunzi katika Idara ya Uhandisi Mitambo, nasimama mbele yako nikiwa na shukrani na shangwe kusherehekea hatua hii muhimu. Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa Mpango wa Kujitolea wa KOICA, hasa mfanyakazi wa kujitolea wa DMD, Hyungmun Lee, kwa ujuzi wake wa ajabu na kwa kubadilisha chuo chetu kupitia utoaji wa vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia."

Mwakitaja aliendelea, "Msaada wako na imani katika uwezo wetu imetupa miguu mahiri ya uhandisi kuwa kabla ya wakati na mabawa madhubuti ya kitaaluma kuwa juu."

"Maabara hii inawezesha zaidi ya studio ya kubuni tu. Ni mwanga wa matumaini ya kitaaluma, ujuzi na maendeleo - hali ya uvumbuzi na ushahidi wa kile ambacho urafiki wa ATC na KOICA unaweza kufikia. Maabara hii itakuwa darasa letu, warsha yetu, na uzinduzi wetu. Itatupa uwezo wa kukabiliana na changamoto za ulimwengu halisi, kutoka kwa kubuni nyenzo za kiteknolojia na teknolojia endelevu."














Ends...

Post a Comment

0 Comments