IKOMBA, AKOMBA KURA KIBAO UWENYEKITI CWT,AMGARAGAZA VIBAYA MWALIMU LEAH MTETEZI WA KITI HICHO

 By arushadigtal -DODOMA 


Hatimaye tambo na majigambo ya wagombea nafasi ya Rais Chama cha Walimu Tanzania (CWT) zimekwisha baada Mwalimu Suleiman Ikomba kutangazwa mshindi akimbwaga kwa mbali aliyekuwa Rais wa chama hicho Mwalimu Leah Ulaya.


Wawili hao walikuwa wamevuta hisia za Walimu na Watanzania kwa ujumla kutokana na nafasi walizokuwa wakizishirikia awali ya mmoja kuwa Rais na Mwingine makamu wa Rais.

 

Tambo za wagombea hao zilisikika mitaani na ndani ya Ukumbi wa Jakaya Kikwete ambao kwa siku tatu ulikuwa na Ulinzi mkali kila kona wa Jeshi la polisi pamoja na Suma JKT.

 

Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi huo Halima Liveta amemtangaza hayo alfajiri ya leo Suleiman Mathew Ikomba kuwa amepata kura 608 dhidi ya kura 260 alizozipata aliyekuwa Rais wa awamu iliyopita Leah Ulaya wakati kura moja ikiharibika.

 

Hata hivyo, amesema jumla ya wapiga kura walioripoti kwenye uchaguzi huo walikuwa 914 lakini waliopiga kura walikuwa 868.

Post a Comment

0 Comments