#UGANDA: OFISI YA DPP UGANDA YADAI BESIGYE ALIPANGA NJAMA ZA MAUAJI YA RAIS MUSEVENI
By arushadigtal-UGANDA
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Dkt Kizza Besigye ametuhumiwa kupanga njama ya kumuua Rais Yoweri Museveni kwa kutumia ndege zisizo na rubani na sumu ya ricin.
Madai hayo yaliwasilishwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) mahakamani kama sehemu ya kesi ya uhaini dhidi ya Besigye na washtakiwa wengine wawili: Obeid Lutale na Kapteni Denis Oola.
Madai hayo yamezua taharuki kubwa ya kisiasa nchini Uganda, huku wengi wakiyaona kama mbinu ya kukandamiza upinzani.
Besigye, mkosoaji wa muda mrefu wa Museveni, amekanusha vikali madai hayo, akidai kuwa hayana msingi na yana msukumo wa kisiasa.
0 Comments